0
Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia na MAendeleo (CHADEMA), Freeman Mbowe amesema nguvu na umoja wa UKWA vilivyopo sasa vitaendelea kuwepo na kutumika hadi katika uchaguzi mkuu wa mwaka 2015.

Mbowe alitoa kauli hiyo jana kwenye mkutano mkuu wa sita wa Chama cha Wananchi (CUF), unaoendelea katika Ukumbi wa Blue Pearl jijini Dar es Salaam.

Akisisitiza zaidi Mbowe alisema “ushirikiano wa UKAWA si wa kupita na wala hautaishia kwenye mchakato wa katiba mpya. Umoja huu unapaswa kuundiwa mkakati ili kuudumisha.”

Post a Comment

 
Top