0
Mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania, Mbwana Samatta ambaye kwa sasa anachechezea klabu ya TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, yuko katika mipango ya kuhamia Ulaya. Taarifa za uhakika zinasema Samatta tayari ameshamtaarifu uamuzi wake huo tajiri wa timu hiyo, Moisse Katumbi Chapwe, ambaye amekubaliana naye.

Aidha, pamoja na kutokutaka kkuelezea klabu za Ulaya zinazomuwania Samatta amedokeza kuwa anatarajia kucheza Ufaransa, Ureno au Ubelgiji kulingana na makubaliano yatakavyofikiwa.

Post a Comment

 
Top