
YANGA SC NA BATA BULLETS JUMAPILI TAIFA
Yanga
SC itashuka tena dimbani Jumapili kumenyana na Bata Bullets ya Malawi
katika mchezo wa kirafiki Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Huo utakuwa
mchezo wa tano chini ya kocha mpya, Mbrazil Marcio Maximo baada ya awali
kushinda mechi zote nne, 1-0 mara mbili dhidi ya Thika United ya Kenya
na Chipukizi ya Pemba na 2-0 mara mbili dhidi ya Shangani na KMKM zote
za Zanzibar. Yanga SC imetoa wito kwa mashabiki wake kujitokeza kwa
wingi kwenye mchezo huo Jumapili kuipa sapoti timu yao.

Post a Comment